TUME Logo
TUME Logo
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Tume ya Kuchunguza Matukio Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025

Balozi David Joseph Kapya

David Joseph Kapya photo
Balozi David Joseph Kapya
Mjumbe wa Tume

Barua pepe: katibu@tume.uchunguzi.go.tz

Simu: 0743 040 890

Wasifu

Balozi David Joseph Kapya, ni Balozi na mwanadiplomasia mwandamizi ambaye amewahi kuwa msaidizi mahususi wa Rais wa awamu ya tatu Hayati Benjamin Willium Mkapa katika mazungumzo ya kutatua migogoro na kuleta amani mashariki ya DRC, amekuwa msaidizi mahususi wa Rais wa awamu ya tatu katika usuluhishi wa mgogoro wa Sudan, juhudi ambazo zilipelekea kuzaliwa kwa taifa jipya la Sudan Kusini. Amekuwa mshauri mahususi wa Rais wa awamu ya tatu katika upatanishi wa mgogoro wa kisiasa nchini Burundi, awahi kuwa mdaidizi mahususi wa rais wa awamu ya nne Mhe. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete katika timu ya Umoja wa Afrika ya Usuluhishi wa Mgogoro Nchini Ivory Coast, na amewahi kuwa mwakilishi maalum wa Tanzania kwenye utatuzi wa mgogoro wa kisiasa nchini Zimbambwe.

Wasiliana Nasi